Friday, October 21, 2016

Teknomiles - Diana [Official Video].....


New Video Teknomiles-Diana

Nguli wa muziki wa afro jazz Kenya Achieng Abura afariki dunia...



Achieng AburaImage copyrightACHIENG ABURA / FACEBOOK
Image captionAchieng Abura alishinda tuzo ya Kora mwaka 2004

Mwanamuziki nguli wa nyimbo za mtindo wa Afro Jazz kutoka Kenya Achieng Abura amefariki dunia.
Mwanamuziki huyo aliaga dunia akipokea matibabu katika hospitali kuu ya taifa ya Kenyatta (KNH) jijini Nairobi.
Lydia Achieng Abura, alipata umaarufu miaka ya 1990 kwa wimbo wa injili kwa jina I Believe.
Baadaye, alianza kukumbatia mitindo mingine ya uimbaji kama vile jazz.
Kwenye ujumbe katika ukurasa wa Facebook mapema mwezi huu, alikuwa amedokeza kwamba hakuwa buheri wa afya.
Alisema alikuwa amepoteza uzani wa kilo 50 katika kipindi cha miaka mitatu pekee, na madaktari walikuwa wamemshauri kuongeza uzani.
"Kutembea ni shida na ninaumwa kila pahali," aliandika.

Achieng AburaImage copyrightACHIENG ABURA / FACEBOOK

Kwenye mahojiano na gazeti la Business Daily mwezi Julai, alikuwa amesema alikabiliwa na matatizo ya kifedha kutokana na afya ya mwanawe wa kiume aliyehitaji kufanyiwa matibabu ambayo yangegharimu Sh4 milioni (dola 400,000 za Marekani).
"Niliandaa mchango lakini waliohudhuria walikuwa chini ya 10," aliambia gazeti hilo.
Abura alishinda tuzo ya muziki ya Kora mwaka 2004.
Alikuwa pia jaji katika shindano la kuwatafuta wanamuziki wenye vipaji la Tusker Project Fame ambalo liliwashirikisha vijana kutoka nchi za Afrika Mashariki.
Wanamuziki wenzake, viongozi na mashabiki wameeleza kushangazwa kwao na kifo hicho na wamekuwa wakituma salamu za rambirambi mtandaoni.

Suzanna OwiyoImage copyrightTWITTER
Sauti SolImage copyrightTWITTER

AliKiba na Mr Blue waungana kwajili ya Abby Skills.....

Msanii ambaye alifanya vizuri kipindi cha nyuma na nyimbo ‘Maria’ na ‘Mimi na Wewe’ Abby Skills anajipanga kurudi upya katika game la muziki na wimbo ‘Averina’ akiwa na Ali Kiba.
Image result for alikiba na mr. blue
Muimbaji huyo ameiambia Bongo5 kuwa AliKiba na Mr Blue ndiyo watu ambao wanamsimia kwa sasa ili kumrudisha upya kwenye chati.
“AliKiba na Mr Blue walikaa chini na kuamua kunisaidia kunirudisha kwenye game,” alisema Abby. “Waliniambia tumeona una kipaji kizuri, una melody ngoja tushirikiane ili kukupeleke sehemu fulani,”
Aliongeza, “Hata hii project yangu mpya na AliKiba ‘Averina’ wao ndio wanasimamia kila kitu, kwa hiyo kuna mambo mazuri yanakuja hivi karibuni,”
Muimbaji huyo amesema kazi yake mpya aliyomshirikisha AliKiba itatoka hivi karibuni kwa kuwa tayari ameshashoot na video.

Thursday, October 20, 2016

MBWA ALIYE DUNGWA MSUMARI KICHWANI LAKINI AWA HAI....


Mbwa azikwa akiwa hai huku akiwa amedungwa msumari kichwani
Image captionMbwa azikwa akiwa hai huku akiwa amedungwa msumari kichwani
Mbwa mmoja amepatikana amezikwa akiwa hai huku msumari ukiwa umedungwa kichwani mwake katika eneo la Teesside katika kile shirika linalokabiliana na unyanyasaji wa wanyama nchini Uingereza RSPCA linasema ni kitendo cha ukatili.
Wanandoa wawili waliokuwa wakitembea katika eneo la Kirkleatham Wood ,walisikia kilio cha kitu kilichokuwa kikilia kwa uchungu na kumpata mbwa huyo ambaye tayari alikuwa amezikwa.
Alikimbizwa kwa daktari wa wanyama lakini majeraha yake mabaya yalimlazimu mtabibu huyo kumuua.
Shirika hilo la wanyama linasema kuwa zaidi ya mtu mmoja alihusika katika kitendo hicho.
Inspekta Nick Jones alisema: katika kipindi cha miaka kumi ambacho nimefanyia kazi RSPCA,sijawahi kuona kitu cha kuogofya na ukatili mkubwa kama huu.

Sunday, October 2, 2016

Yaliyotokea siku kama ya leo katika historia duniani tarehe 02 octoba.....



Siku kama ya leo miaka 147 iliyopita, alizaliwa Mahatma Gandhi, kiongozi wa harakati ya kupigania uhuru nchini India katika moja ya vijiji vya jimbo la Gujarat. Mwaka 1891.Gandhi alirejea kutoka nchini Uingereza na kuishi mjini Mumbai. Mwaka 1893 Mahatma Gandhi alielekea mjini KwaZulu-Natal nchini Afrika Kusini. Akiwa nchini humo alishuhudia ubaguzi wa rangi wa jamii ya wachache ndani ya taifa hilo. Mwaka 1917 na baada ya kurejea nchini kwake alipata umashuhuri mkubwa. Na miaka michache baada ya Vita vya Kwanza na vya Pili vya Dunia yaani akiwa na umri wa miaka 33 aliongoza mapambano kwa ajili ya kuwaokoa watu wake sanjari na kupigania uhuru wa India kutoka mikononi mwa Waingereza ambapo hatimaye na baada ya kuvumilia matatizo mengi tofauti kama vile Jawaharlal Nehru akafanikiwa kulipatia uhuru taifa hilo hapo mwaka 1947.
Siku kama ya leo miaka 112 iliyopita sawa na tarehe Pili Oktoba 1904, alizaliwa Graham Greene mwandishi wa Uingereza. Siku zote mwandishi huyo aliakisi matendo mema na mabaya katika athari zake na aliandika kwenye kitabu chake kinachoitwa 'Nguvu na Utukufu' kwamba subira, uvumilivu na mateso ni njia ya wokovu. Graham Greene ameacha vitabu vingi ambapo baadhi ni 'Mtu wa Tatu', 'Utawala Unaotisha' na Muuaji wa Kukodishwa'. Mwandishi huyo Muingereza alifariki dunia mwaka 1991.
Siku kama ya leo miaka 58 iliyopita yaani sawa na tarehe Pili Oktoba 1958, nchi ya Guinea Conakry ilifanikiwa kujipatia uhuru wake kutoka kwa mkoloni Mfaransa. Wareno walianza kumiminika nchini Guinea mwishoni mwa karne ya 15, na ilipoanza karne ya 19, Wafaransa wakawa na satua zaidi nchini humo na ulipotimia mwaka 1849, nchi hiyo ikakoloniwa rasmi na Ufaransa. Guinea Conakry inapakana na nchi za Senegal, Mali, Ivory Coast, Liberia, Sierra Leone na Guinea Bissau.

NEW VIDEO; LADY JAY DEE - SAWA NA WAO [music]


LADY JAY DEE - SAWA NA WAO [music video/audio]