Tuesday, August 30, 2016

NAHREEL: AMWAGA SUMU MPYA THE INDUSTRY...


2
Mtaarishaji bora wa music nchini Tanzania 2015-2016 EMMANUEL MKONO Maarufu kama NAHREEL sasa yupo mbioni kuibua vipaji vipya katika tasnia hiyo ya utaarishaji wa muziki Nchini Tanzania.
Mtaalishaji huyo ambaye pia ni  C.E.O wa Label ya The industry Tz amesema hayo mara baada ya kuwasili jana siku ya jumatatu ktk makazi yake jijini Dar es salaam kutoka katika moja ya tour za fiesta zinazoendelea katika mikoa tofauti nchini Tanzania
“Mmmh nafikiri ni mapema sana kuzungumzia hilo ila!!!! Yaah kuna watu ninao tayari na tayari tameanza kuealekezana vitu vichache kuhusu production,walikuja wengi,   zaidi ya  ishirini lakini tukaangalia wale ambao tunaweza kuwa nao na kuelekezana vitu vichache tu but now nipo na hiyo project na nta introduce itapofika wakati soon” alisema Nahreel
Pia amewakumbusha mashabiki wa navy kenzo na The industry kwa ujumla kuwa sasa wanaweza kupata taarifa za label hiyo kwa kudownload APP TIMA (The Industry Music App) ambayo itawasaidia kupata taarifa za kipekee


No comments:

Post a Comment