Saturday, August 6, 2016

Vifo vya watu 13 kwenye Bar Ufaransa........


Wakati nchi ya Ufaransa ikiwa kwenye ulinzi mkali kutokana na mashambulizi kadhaa ya kigaidi hivi karibuni ikiwemo mauaji ya mchungaji katika mji mdogo karibu na Rouen.
August 6 2016 imeripotiwa kutokea kwa moto kwenye bar moja kaskazini mwa Ufaransa kwenye mji wa Rouen na kusababisha vifo vya watu 13 na kujeruhi wengine sita. 
Vyombo vya habari nchini humo vimeeleza kwamba chanzo cha moto huo  ni mshumaa ambao uliwashwa kwenye birthday party ya mtu binafsi iliyokuwa inafanyika ndani ya bar hiyo.

No comments:

Post a Comment