Takwimu hizo zimetolewa na Mkuu wa wilaya ya Dodoma, Christina Mndeme katika ufunguzi wa mafunzo ya ufunguzi wa wasimamizi wa mitihani manispaa ya Dodoma.

“Inasikitisha sana unapopokea taarifa kwa watoto wa kike kupokea mimba, sasa hivi kwa wilaya ya Dodoma kwa shule za sekondari mpaka mwenzi huu wa nane ni mimba 45 kwa shule za sekondari na kwa shule za msingi ni mimba 6,” alisema.
“Ni suala la kusikitisha na kuumiza na ndio maana tunapambana kuhakikisha wilaya hii tunatokomeza suala hili na ndio maana tumekuja kwa kauli mbiu hii ya ‘niache nisome magauni manne.'”
Kuhusu wale waliowapa mimba wanafunzi hao, mkuu huyo wa wilaya alisema wakibainika watakiona cha mtema kuni.
“Kwanza ni kuwakamata wale wote waliohusika kuwapa wanafunzi mimba, kesi ziko polisi kuna wachache wametoroka tunaendelea kuwafuatilia lakini nitoe wito kwa wazazi watoe ushirikiano kwa serikali yao kwasababu kumekuwa na udanganyifu kwa wazazi, hivyo kuwafichia siri wale waliowapa mimba watoto na kuwafundisha kuwakana waliowapa mimba watoto.”
No comments:
Post a Comment