Saturday, July 23, 2016

TOP 5 ya mastaa wa soka waliotokea katika familia za kitajiri....

Soka ni mchezo ambao umekuwa kama mkombozi wa vijana wengi waliotokea katika familia za kimasikini, asilimia kubwa ya wanasoka wanaotamba katika soka kwa viwango vya juu wametokea familia za kimasikini, ila hiyo haimaanishi kuwa hakuna wanasoka waliotokea familia za kitajiri.
July 23 naomba nikusogezee Top 5 ya mastaa wa soka waliotokea familia za kitajiri.
1- Andrea Pirlo zaidi ya mara moja amewahi kunukuliwa na vyombo vya habari akisema kuwa hakuwahi kucheza soka kwa ajili ya kupata fedha ili kujikwamua kimaisha, ila aliamua kucheza soka kwa sababu ndio mchezo aliokuwa anaupenda.
Andrea-Pirlo-Wallpapers
Andrea Pirlo
2- Gerard Piqué wa FC Barcelona historia yake na shule aliyosoma kwao Hispaniainatosha kujua ni kijana aliyetoka katika familia ya inayojiweza, Pique amesoma shule ambayo hawasomi watoto wanaotokea katika familia za chini, hiyo inatokana na gharama ya ada katika shule hiyo.
maxresdefault
Gerard Piqué
3- Robin Van Persie huyu anatajwa kuwa toka yupo mdogo aliamua kuwaambia wazazi wake kuwa anataka kuwa mwanasoka, kitu ambacho hakikuwa kigumu kupata sapoti ya kila kitu kwa familia yake kulingana na kwao kuwa na uwezo, ni mwanasoka ambaye hakuwahi kucheza soka peku kama Luis Suarez.
Elko-11
Robin Van Persie
4- Diego Forlán mshambuliaji huyu wa kimataifa wa Uruguay ambaye amewahi kuzichezea  Atletico Madrid na Man United, tangu  mtoto aliwahi kuwaambia wazazi wake kutokana na kuwa na kipato waunde mfuko wa kuwasaidia watu wasiojiweza.
diegoforlan-cropped_1f5zls9ijtv871nhyc16j2vjwt
Diego Forlán
5- Ricardo Kaka huyu ndio mbrazil wa mwisho kushinda tuzo ya mchezaji bora wa duniaBallon d’Or 2007 na ndio mchezaji pekee aliyewahi kushinda tuzo hiyo mbele yaRonaldo na MessiKaka hakutokea familia ya kimasikini kama ilivyo kwa mbrazil mwenzake Ronaldo de Lima, baba yake alikuwa injinia na kaka zake walikuwa wameshafanikiwa katika soka.

No comments:

Post a Comment