Friday, July 22, 2016

Zoezi la uhakiki wa silaha jiji Dar es salam lamazikiza


Polisi kanda maalum ya Dar es salaam leo July 22 2016  wametoa majumuisho ya zoezi la uhakiki wa silaha mkoa wa Dar es salaam lililofanyika kwa miezi mitatu, zoezi hilo lilianza March 1 2016 na limemalizika June 30 2016.
Kamishna wa polisi kanda maalumu ya Dar es salaam, Simon Sirro ametoa taarifa hiyo mbele ya wandishi wa habari na kusema idadi ya watu waliojitokeza kuhakiki silaha kwa wilaya zote tatu ni 11,602 na jumla ya silaha 14107 zilihakikiwa.
Jumla ya silaha 66 zilisalimishwa kutokana sababu mbalimbali ikiwamo mmiliki wa silaha kuwa na umri mkubwa na kushindwa kumudu silaha. Zoezi la uhakiki wa silaha limeiingizia Serikali mapato kiasi cha Mil 198.8

No comments:

Post a Comment