Saturday, July 23, 2016

The Rock ndiye muigizaji wa Hollywood anayelipwa fedha nyingi zaidi

Kutoka kuwa mwanamieleka aliyekuwa na mafanikio makubwa, sasa The Rock ndiye muigizaji wa Hollywood anayelipwa fedha nyingi zaidi, kwa mujibu wa Forbes.
Muigizaji huyo ambaye jina lake halisi ni Dwayne Johnson ameingiza dola milioni 64.5 mwaka huu. Johnson amepanda kutoka dola milioni 31.5 alizoingiza mwaka jana.
dwayne-johnson-the-rock-2014-billboard-650
The Rock alikamata nafasi ya 19 kwenye orodha ya Forbes ya mastaa wanaolipwa fedha nyingi zaidi mwaka huu na kuongozwa na Taylor Swift, aliyeingiza dola milioni 170.

No comments:

Post a Comment