Friday, July 22, 2016

Koffie Olomide amdunda dancer wake wa kike airport Nairobi

Mwanamuziki mkongwe wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Koffie Olomide amejikuta kwenye skendo akitua kwenye uwanja wa ndege kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi, Kenya na kuonekana akimpiga dancer wake wa kike.
Muimbaji huyo anayetarajiwa kutumbuiza kwenye viwanja vya Bomas of Kenya, Jumamosi hii anaonekana kwenye video iliyonaswa akimpiga teke dancer wake.

Kwa mujibu wa vyanzo, dancer huyo anadaiwa kumkosea heshima mpenzi wake Cindy Le Couer ambaye ni muimbaji wa bendi yake. Bado Olomide anaishi na mke wake Aliane Olomide ambaye amezaa watoto saba naye.
Kwa mujibu wa Xavier Jerry Nato, hivi ndivyo mkasa ulivyokuwa.www.voicekitaatz.blogspt.com

No comments:

Post a Comment