Friday, July 22, 2016

Mtando mpya TZ


Ezylinc ni mtandao mpya wa kijamii, ambapo watu binafsi na makampuni wanaweza kuweka
picha na kuandika makala kuhusu vivutio vya utalii vilivyopo nchini.

Mtu yeyote anaweza kujiunga na mtandao huu wa kijamii bure kabisa kwa kujisajili
www.ezylinc.com , baada ya hapo anaweza kuweza picha, kuandika makala kuhusu vivutio vya
utalii, kutengeneza magroup, kukutana na marafiki wengi zaidi kutoka sehemu mbalimbali
duniani na mengine mengi.

Ezylinc inaunganisha makundi mawili. Upande mmoja tuna watalii, na kwa upande mwingine
watu wanaofanya kazi zinazoendana na shughuli za kitalii.

Hapa Tanzania kama mfano, utalii ni sekta inayoliingizia taifa fedha nyingi za kigeni. Katika mwaka
2014 sekta ya utalii, imechangia asilimia 17 katika pato la taifa na kuchangia kwa asilimia 25 ya
mapato yote ya fedha za kigeni, ambapo bilioni 2 za Kimarekani zilipatikana.

Tanzania ni nchi yenye vivutio vingi vya utalii katika bara la Afrika. Kilimanjaro mlima mrefu kuliko
yote Africa, Visiwa vya Zanzibar, hifadhi za taifa za Serengeti na Ngorongoro, Tarangire, Ziwa
Manyara, Ruaha na Selous, ni mifano hai michache ya vivutio vinavyopatikana Tanzania.

Kwa kutumia mtandao huu mpya wa kijamii tunaweza kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini
kwetu kwa urahisi zaidi, na kupata watalii wengi zaidi.

Hii ni moja ya sababu kubwa kutengeneza mtandao mpya huu wa kijamii. Tunalenga kusaidia
ukuaji zaidi wa sekta ya utalii nchini, na hiyo itasaidia watu wengi zaidi kupata ajira katika shuguli
zinazoendana na sekta hiiwww.voicekitaatz.com

No comments:

Post a Comment