Baada
ya mauaji ya Wamarekani weusi wawili juzi ambayo yamepelekea kuuwawa
kwa Polisi watano kwenye mji wa Dallas Marekani kama njia ya kulipa
kisasi, Wanahiphop maarufu kutoka jimbo la California Marekani The Game na Snoop Dogg wameongoza kundi la Wanaume kwenye matembezi ya amani mpaka makao makuu ya Polisi.
Moja ya post za The Game akisema ‘sisi sio Wanyama’
The Game na Snoop Dogg wakiongoza matembezi ya amani kuelekea makao makuu ya Polisi Los Angeles California.
Kwenye hii movement yao iitwayo H.U.N.T (Hate Us Not Today) viongozi Snoop Dogg na The Game walikutana na uongozi wa Polisi pamoja na Meya wa Los Angeles Eric Garcetti.
The Game amesema ameguswa kufanya hivyo sababu ameona hali inavyoelekea ni kwamba Ubinaadamu unaondoka ndio maana akaamua kutumia ushawishi wake kusaidia kumaliza au kukiondoa kinachotaka kutokea, sisi sio Wanyama.
No comments:
Post a Comment